Mola nipe ujasiri, leo niyaseme wazi,
Ninene yalo dhahiri, masikio yayajazi,
Siitaki iwe siri, sitaki kigugumizi,
Mbeya twataka amani, asotaka aondoke.
Mbeya twataka amani, tumechoka kuonewa,
Mwatuweka kundi gani, la mchwa ama la chawa?
Mmeuguwa vichwani, pengine mpewe dawa,
Mbeya twataka amani, asotaka aondoke.
Asotaka aondoke, Mbeya akatuachia,
Situfanye tuta’bike, mabavu kuyatumia,
Aondoke ende zake, mji uweze tulia,
Mbeya twataka amani, asotaka aondoke.
Mbeya mahali pazuri, wachache wapaharibu,
Vichwani hawafikiri, huongozwa na gadhabu,
Hudhani umashuhuri, jamii kuiadhibu,
Mbeya twataka amani, asotaka aondoke.
Dada kamwambie kaka, avifungashe virago,
Kaseme tumeshachoka, atuondolee zogo,
Amani in’otoweka, aibebee mpago,
Mbeya twataka amani, asotaka aondoke.
Aondoke ende zake, asirudi tena Mbeya,
Kamwe tusimkumbuke, kwa huo wake ubaya,
Sana asahaulike, fikiraze zilopwaya,
Mbeya twataka amani, asotaka aondoke.
Pamoja tushikamane, kuitetea amani,
Kamwe tusivurugane, wabaya wapigwe chini,
Sisi sote tuungane, kuondoa wafitini,
Mbeya twataka amani, asotaka aondoke.
Tuijenge Mbeya yetu, ili izidi kung’aa,
Ili wale waso utu, wabaki kuishangaa,
Na tusikubali katu, Mbeya yetu iwe jaa,
Mbeya twataka amani, asotaka aondoke.
Chonde chonde waungwana, maneno myasikie,
Ubabe wenu hapana, kwingine mkafanyie,
Kwetu hamna maana, si wagomvi watu sie,
Mbeya twataka amani, asotaka aondoke.
Aende afanye hima, atuwekea usiku,
Atwache sisi salama, kwani sisi siyo kuku,
Aende zake mapema, tutamtoa mkuku,
Mbeya twataka amani, asotaka aondoke.
Mimi nimeamua kujitoa mhanga kwa ajili ya kuwaokoa vijana wenzangu. Siogopi hata kufa kwa kusema ukweli.
Amina Chifupa.
1981-2007.
Amina Chifupa.
1981-2007.
Saturday, November 12, 2011
Thursday, November 10, 2011
Mganga wewe mwenyewe
Wa’ngaika kila siku, ukiwasaka waganga,
Waenda kule na huku, umefika hata Tanga,
Mepeleka hadi kuku, ‘lipokwenda Sumbawanga,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Tajihangaisha bure, kudhani wanakuroga,
Mume usimpapure, ukadhani yeye boga,
Mume simcheze shere, kwayo mambo ya kuiga,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Mume usipomtii, lazima atakuchoka,
Kama wewe husikii, ndoa itaharibika,
Na ndoa haikawii, vivi hivi kuvunjika,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Chunga mwenendo wako, uone kama wafaa,
Wacha kufanya vituko, ndoa itakuchakaa,
Sikudanganye wenzako, kwani dunia hadaa,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Mpe mumeo heshima, naye atakuthamini,
Mwambie kwayo hekima, yaliyo mwako moyoni,
Kubali akikutuma, uwache umajinuni,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Usiufate mkumbo, sijaribu asilani,
Yatakuchachia mambo, wenza wacheke pembeni,
Ndoa hainazo tambo, bali busara kichwani,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Mwanamke mpumbavu, hubomoa nyumba yake,
Na mwanamke mvivu, hajui wajibu wake,
Tena hawi msikivu, labda siku atake,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Watu wakikukosoa, ni vema uwaelewe,
Ndoa kiitia doa, talia wewe mwenyewe,
Wengine wataopoa, kutunza usaidiwe,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Waenda kule na huku, umefika hata Tanga,
Mepeleka hadi kuku, ‘lipokwenda Sumbawanga,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Tajihangaisha bure, kudhani wanakuroga,
Mume usimpapure, ukadhani yeye boga,
Mume simcheze shere, kwayo mambo ya kuiga,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Mume usipomtii, lazima atakuchoka,
Kama wewe husikii, ndoa itaharibika,
Na ndoa haikawii, vivi hivi kuvunjika,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Chunga mwenendo wako, uone kama wafaa,
Wacha kufanya vituko, ndoa itakuchakaa,
Sikudanganye wenzako, kwani dunia hadaa,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Mpe mumeo heshima, naye atakuthamini,
Mwambie kwayo hekima, yaliyo mwako moyoni,
Kubali akikutuma, uwache umajinuni,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Usiufate mkumbo, sijaribu asilani,
Yatakuchachia mambo, wenza wacheke pembeni,
Ndoa hainazo tambo, bali busara kichwani,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Mwanamke mpumbavu, hubomoa nyumba yake,
Na mwanamke mvivu, hajui wajibu wake,
Tena hawi msikivu, labda siku atake,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
Watu wakikukosoa, ni vema uwaelewe,
Ndoa kiitia doa, talia wewe mwenyewe,
Wengine wataopoa, kutunza usaidiwe,
Mganga wewe mwenyewe, kunusuru ndoa yako.
maudhui
maisha
Tuesday, November 1, 2011
Leo ni leo
Kesho kesho ya manyani, wangali hawajajenga,
Ilitokea zamani, nyani nao wakapanga,
Wataka wakae ndani, waache kutangatanga,
Wakaiweka yamini, sasa kipigwe kipenga.
Mwingine kakosekana, wakabaki jiuliza,
Akawasili mchana, kisa akawaeleza,
Mtoto kaugua sana, ikabidi kumwuguza,
“Kesho kwa mapema sana, jambo tutatekeleza”.
Kesho ilipofikia, manyani wakajihimu,
Mwenzao hajatokea, ikawajaza wazimu,
Walipomuulizia, mtotowe kanywa sumu,
Nyani wakajiambia, “basi kesho tulazimu”.
Na kesho kulipokucha, mwenzao haonekani,
Wakadhani kawakacha, kemua nenda mitini,
Mwenzao hakujificha, kewa’leza kulikoni,
Amejikwaa ukucha, damu yatoka doleni.
Nyani sasa wakasema, “hebu tusikilizane”,
Kesho yaenda mrama, na mambo yashindikane,
Tuitumie hekima, mambo haya tupangane,
Mwingine akalalama, vema tusubiriane.
Basi hadi leo hii, nyani wasubiri kesho,
Kesho haiwafikii, pengine yao ‘spesho’,
Sasa hawafikirii, weshaona ni michosho,
Pori hawalikimbii, huko sasa kwao mwisho.
Leo ni leo sikia, asemaye kesho mwongo,
Leo leo ngetumia, kuuchekecha ubongo,
Sipende kusubiria, kesho ufanye mipango,
Kesho haitofikia, hata ngetegea ‘mingle’.
Usiwe kama manyani, hukosi visingizio,
Ziweke vema ‘plan’, yanowezekana leo,
Chekecha vema kichwani, kabla yake machweo,
Tena singoje jioni, muda huu egemeo.
Leo iwe yako ada, kesho siisubirie,
Utumie vema muda, kesho ukusaidie,
Kesho ngeipaka poda, bado situmainie,
Leo hainayo shida, siku yako itumie.
Ilitokea zamani, nyani nao wakapanga,
Wataka wakae ndani, waache kutangatanga,
Wakaiweka yamini, sasa kipigwe kipenga.
Mwingine kakosekana, wakabaki jiuliza,
Akawasili mchana, kisa akawaeleza,
Mtoto kaugua sana, ikabidi kumwuguza,
“Kesho kwa mapema sana, jambo tutatekeleza”.
Kesho ilipofikia, manyani wakajihimu,
Mwenzao hajatokea, ikawajaza wazimu,
Walipomuulizia, mtotowe kanywa sumu,
Nyani wakajiambia, “basi kesho tulazimu”.
Na kesho kulipokucha, mwenzao haonekani,
Wakadhani kawakacha, kemua nenda mitini,
Mwenzao hakujificha, kewa’leza kulikoni,
Amejikwaa ukucha, damu yatoka doleni.
Nyani sasa wakasema, “hebu tusikilizane”,
Kesho yaenda mrama, na mambo yashindikane,
Tuitumie hekima, mambo haya tupangane,
Mwingine akalalama, vema tusubiriane.
Basi hadi leo hii, nyani wasubiri kesho,
Kesho haiwafikii, pengine yao ‘spesho’,
Sasa hawafikirii, weshaona ni michosho,
Pori hawalikimbii, huko sasa kwao mwisho.
Leo ni leo sikia, asemaye kesho mwongo,
Leo leo ngetumia, kuuchekecha ubongo,
Sipende kusubiria, kesho ufanye mipango,
Kesho haitofikia, hata ngetegea ‘mingle’.
Usiwe kama manyani, hukosi visingizio,
Ziweke vema ‘plan’, yanowezekana leo,
Chekecha vema kichwani, kabla yake machweo,
Tena singoje jioni, muda huu egemeo.
Leo iwe yako ada, kesho siisubirie,
Utumie vema muda, kesho ukusaidie,
Kesho ngeipaka poda, bado situmainie,
Leo hainayo shida, siku yako itumie.
maudhui
maisha
Sunday, October 30, 2011
Niheshimu nikweshimu
Fanya nawe nitendee, unalopenda tendewa,
Maneno unisemee, unayopenda semewa,
Ikibidi nichekee, kama wapenda chekewa,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Jambo usilolitaka, nami usinifanyie,
Uniombee baraka, visa usinitilie,
Usiwe wa kuropoka, bali mema unambie,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Usiwe wa kulalama, jambo usipofanyiwa,
Bali uchunguwe vema, kama huwa wajitowa,
Kiasi unachopima, ndicho hicho tapimiwa,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Ukitaka sikilizwa, wengine wasikilize,
Ili kama ni kutuzwa, nawe wengine watuze,
Vinginevyo utalizwa, na watu wakuzeveze,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Cha kwangu ukikitaka, isiwe chako waficha,
Kwangu ukila nafaka, kwako sinilishe kucha,
Nikikupa vya kuoka, nigee japo mchicha,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Wepesi wa kupokea, uwe na kwenye kutoa,
Kitu mtu kikugea, wewe sibaki kodoa,
Nawe kimpelekea, upamoja hutopoa,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Heshima ninayokupa, nawe uitoe pia,
Siyo wewe unakwepa, huku yangu watakia,
Sinifanye kukwogopa, daima kunitishia,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Maneno unisemee, unayopenda semewa,
Ikibidi nichekee, kama wapenda chekewa,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Jambo usilolitaka, nami usinifanyie,
Uniombee baraka, visa usinitilie,
Usiwe wa kuropoka, bali mema unambie,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Usiwe wa kulalama, jambo usipofanyiwa,
Bali uchunguwe vema, kama huwa wajitowa,
Kiasi unachopima, ndicho hicho tapimiwa,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Ukitaka sikilizwa, wengine wasikilize,
Ili kama ni kutuzwa, nawe wengine watuze,
Vinginevyo utalizwa, na watu wakuzeveze,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Cha kwangu ukikitaka, isiwe chako waficha,
Kwangu ukila nafaka, kwako sinilishe kucha,
Nikikupa vya kuoka, nigee japo mchicha,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Wepesi wa kupokea, uwe na kwenye kutoa,
Kitu mtu kikugea, wewe sibaki kodoa,
Nawe kimpelekea, upamoja hutopoa,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Heshima ninayokupa, nawe uitoe pia,
Siyo wewe unakwepa, huku yangu watakia,
Sinifanye kukwogopa, daima kunitishia,
Niheshimu nikweshimu, unipende nikupende.
Saturday, October 29, 2011
Kiburi si maungwana
“Sitaki mimi sitaki”, wakubwa wawaambia,
Mtoto haushikiki, huna unalo sikia,
Na wala huambiliki, ungali hujatulia,
Kiburi si maungwana.
Wauleta ukaidi, wakubwa kuwoneshea,
Kamwe huwezi faidi, wote watakukimbia,
Hata ingefika “Eid”, tabaki kuisikia,
Kiburi si maungwana.
Wakubwa husikilizi, wataka jiamulia,
Jambo hawakuelezi, kiambiwa wachukia,
Wajipa wewe ujuzi, huna usilolijua,
Kiburi si maungwana.
Maneno yako makali, daima wayatumia,
Nywelezo kipilipili, kucha unasimamia,
Hunayo ardhilhali, busara mekuishia,
Kiburi si maungwana.
Dunia rangi rangile, kama hukulitambua,
Dunia mwendo mwendole, takuja kukuumbua,
Dunia cheko chekole, hekima ukiijua,
Kiburi si maungwana.
Kiburi chako kiwache, hata Mungu achukia,
Tabiayo ipekeche, watu kuifurahia,
Mabayayo uyafiche, jalala kuyatupia,
Kiburi si maungwana.
Mtoto haushikiki, huna unalo sikia,
Na wala huambiliki, ungali hujatulia,
Kiburi si maungwana.
Wauleta ukaidi, wakubwa kuwoneshea,
Kamwe huwezi faidi, wote watakukimbia,
Hata ingefika “Eid”, tabaki kuisikia,
Kiburi si maungwana.
Wakubwa husikilizi, wataka jiamulia,
Jambo hawakuelezi, kiambiwa wachukia,
Wajipa wewe ujuzi, huna usilolijua,
Kiburi si maungwana.
Maneno yako makali, daima wayatumia,
Nywelezo kipilipili, kucha unasimamia,
Hunayo ardhilhali, busara mekuishia,
Kiburi si maungwana.
Dunia rangi rangile, kama hukulitambua,
Dunia mwendo mwendole, takuja kukuumbua,
Dunia cheko chekole, hekima ukiijua,
Kiburi si maungwana.
Kiburi chako kiwache, hata Mungu achukia,
Tabiayo ipekeche, watu kuifurahia,
Mabayayo uyafiche, jalala kuyatupia,
Kiburi si maungwana.
Friday, October 28, 2011
Mungu akisema ndiyo
Maisha ni mbio mbio, hayanayo lelemama,
Ujapo uamkio, kujihimu kwa mapema,
Ushike kitafutio, usibaki kulalama,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Maisha ni harakati, riziki jitafutia,
Uchakarike ‘usweti’, mahali kupafikia,
Uchungu wa mkuyati, nao ukakuingia,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Katika mafanikio, hawakosi maadui,
Wale wafikiriao, kukutenda ubedui,
Wa mapembe masikio, nazo roho za utui,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Wa nukhsi nukhsani, mambo kukuharibia,
Wanoumia rohoni, mambo yakikunyokea,
Watemao mate chini, ukishaipita njia,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Wenye husuda rohoni, pindi ukifanikiwa,
Wenye kusema pembeni, ati umependelewa,
Daima wanotamani, wewe kuharibikiwa,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Wakeshao kwa waganga, kukufanyia mizungu,
Ili uweze boronga, maisha yawe machungu,
Wasochoka kusimanga, kukuwekea kiwingu,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Hakuna wa kuzuia, Mungu akishaamua,
Baraka kikujazia, wengine wajisumbua,
Watabaki kuumia, roho zikiwatufua,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Milango ‘kikufungia, siache kumwomba Mungu,
Yeye takufungulia, kokote chini ya mbingu,
Kheri atakujazia, hata iwe kwa mafungu,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Jifunze sana subira, ila sikose imani,
Omba sana kwa busara, umwombe yeye Manani,
Akwepushie madhara, na roho za wafitini,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Visa wakikufanyia, kamwe siwarudhishie,
Mola atakujalia, mabaya akwepushie,
Baya kikusingizia, Mola akusaidie,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Watahangaika bure, kama Mungu keshasema,
Vyao ni viherehere, na roho zikiwauma,
Waachie ziwafure, wewe zidi tenda mema,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Tayezuia ni nani, Mungu kishakuchagua,
Hawawezi abadani, wakeshe wakiagua,
Mungu siye Athumani, kila mtu amjua,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Usije kata tamaa, kisa wenye roho mbaya,
Waufanyao unaa, mambo kuharibikiya,
Wakwombeao balaa, waache waule chuya,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Hakuna wa kuzuia, Mungu akisema ndiyo,
Ukweli nimekwambia, kaziyo kujua hayo,
Yalo mema simamia, Mola ndiyo kimbiliyo,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Ujapo uamkio, kujihimu kwa mapema,
Ushike kitafutio, usibaki kulalama,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Maisha ni harakati, riziki jitafutia,
Uchakarike ‘usweti’, mahali kupafikia,
Uchungu wa mkuyati, nao ukakuingia,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Katika mafanikio, hawakosi maadui,
Wale wafikiriao, kukutenda ubedui,
Wa mapembe masikio, nazo roho za utui,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Wa nukhsi nukhsani, mambo kukuharibia,
Wanoumia rohoni, mambo yakikunyokea,
Watemao mate chini, ukishaipita njia,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Wenye husuda rohoni, pindi ukifanikiwa,
Wenye kusema pembeni, ati umependelewa,
Daima wanotamani, wewe kuharibikiwa,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Wakeshao kwa waganga, kukufanyia mizungu,
Ili uweze boronga, maisha yawe machungu,
Wasochoka kusimanga, kukuwekea kiwingu,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Hakuna wa kuzuia, Mungu akishaamua,
Baraka kikujazia, wengine wajisumbua,
Watabaki kuumia, roho zikiwatufua,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Milango ‘kikufungia, siache kumwomba Mungu,
Yeye takufungulia, kokote chini ya mbingu,
Kheri atakujazia, hata iwe kwa mafungu,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Jifunze sana subira, ila sikose imani,
Omba sana kwa busara, umwombe yeye Manani,
Akwepushie madhara, na roho za wafitini,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Visa wakikufanyia, kamwe siwarudhishie,
Mola atakujalia, mabaya akwepushie,
Baya kikusingizia, Mola akusaidie,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Watahangaika bure, kama Mungu keshasema,
Vyao ni viherehere, na roho zikiwauma,
Waachie ziwafure, wewe zidi tenda mema,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Tayezuia ni nani, Mungu kishakuchagua,
Hawawezi abadani, wakeshe wakiagua,
Mungu siye Athumani, kila mtu amjua,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Usije kata tamaa, kisa wenye roho mbaya,
Waufanyao unaa, mambo kuharibikiya,
Wakwombeao balaa, waache waule chuya,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Hakuna wa kuzuia, Mungu akisema ndiyo,
Ukweli nimekwambia, kaziyo kujua hayo,
Yalo mema simamia, Mola ndiyo kimbiliyo,
Mungu akisema ndiyo, hakuna wa kuzuia.
Thursday, October 27, 2011
Ukipenda boga
Pendo pendo mwapendana, nyie ni nyie wawili,
Pendo pendo mwashibana, lenu la jambo muhali,
Mwanoga mwaambiana, mwingine hatobadili,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Mapenzi yake matamu, wanogewa na mumeo,
Kamwe haiishi hamu, ana upya kila leo,
Penzi lashika hatamu, huwajali visemeo,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Mumeo umemkuta, anao na ndugu zake,
Binti unafurukuta, hutaki kwako wafike,
Wataka mume kufyata, lako tu nd’o alishike,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Siyo vema mwanakwetu, si tabia yenye sudi,
Nao waoneshe utu, upendo kwao si budi,
Mabezo si malikitu, siwoneshe ukaidi,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Kwa mumeo umekuta, tayari alishazaa,
Kabla hajakupata, akupe wake wasaa,
Mtoto wamkorota, zaidi wamkataa,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Nawe umepata mke, tayari ana mtoto,
Simfanye ateseke, kuiweka nyumba joto,
Haki yake apendeke, siyo kuleta fukuto,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Usipende nusu nusu, nani tena wamwachia,
Yake yote yakuhusu, nayo uyapende pia,
Sisite kumruhusu, nduguze kutembelea,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Mapenzi huleta raha, kwa dhati mkipendana,
Tena huipata siha, kama mwasikilizana,
Siyafanyie mzaha, mkaja kuumizana,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Cha mwenziyo kyone chako, halafu ukithamini,
Kipende moyoni mwako, sikitenge asilani,
Sikifanyie vituko, kamwe kamwe abadani,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Ya kusema nimesema, ni vema kuyasikia,
Yatunze yaliyo mema, kazi ukayafanyia,
Pendo lijae hekima, nyote kulifurahia,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Pendo pendo mwashibana, lenu la jambo muhali,
Mwanoga mwaambiana, mwingine hatobadili,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Mapenzi yake matamu, wanogewa na mumeo,
Kamwe haiishi hamu, ana upya kila leo,
Penzi lashika hatamu, huwajali visemeo,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Mumeo umemkuta, anao na ndugu zake,
Binti unafurukuta, hutaki kwako wafike,
Wataka mume kufyata, lako tu nd’o alishike,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Siyo vema mwanakwetu, si tabia yenye sudi,
Nao waoneshe utu, upendo kwao si budi,
Mabezo si malikitu, siwoneshe ukaidi,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Kwa mumeo umekuta, tayari alishazaa,
Kabla hajakupata, akupe wake wasaa,
Mtoto wamkorota, zaidi wamkataa,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Nawe umepata mke, tayari ana mtoto,
Simfanye ateseke, kuiweka nyumba joto,
Haki yake apendeke, siyo kuleta fukuto,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Usipende nusu nusu, nani tena wamwachia,
Yake yote yakuhusu, nayo uyapende pia,
Sisite kumruhusu, nduguze kutembelea,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Mapenzi huleta raha, kwa dhati mkipendana,
Tena huipata siha, kama mwasikilizana,
Siyafanyie mzaha, mkaja kuumizana,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Cha mwenziyo kyone chako, halafu ukithamini,
Kipende moyoni mwako, sikitenge asilani,
Sikifanyie vituko, kamwe kamwe abadani,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Ya kusema nimesema, ni vema kuyasikia,
Yatunze yaliyo mema, kazi ukayafanyia,
Pendo lijae hekima, nyote kulifurahia,
Basi ukipenda boga, lipende na ua lake.
Wednesday, October 26, 2011
Nifanyeje uridhike?
Chonde chonde niambie, nini unachokitaka,
Kingine nikufanyie, ambacho utaridhika,
Niambie nitulie, nimechoka kuteseka,
Nifanyeje uridhike, nambie basi nijue.
Ulitaka yako nyumba, nyumba nayo nikajenga,
Mkopo nikaubamba, wewe uache kupanga,
Ukakataa Kibamba, hutaki wala Ukonga,
Ukataka Mikocheni, nikakopa uridhike.
Nikasema njoo Mbeya, haraka ukakataa,
Ukadai ni kubaya, wataka kuishi Dar,
Nami nikasema haya, nikuridhishe haswaa,
Bado wataka Ulaya, Dar hapajakufaa.
Mara ukataka gari, huzitaki daladala,
Tena gari la fahari, hutaki hizo Corolla,
Nikuridhishe vizuri, nikaenda kopa hela,
Gari umeshalipata, wasema hujaridhika.
Nguo nzuri uzipate, likawa lako sharti,
Tena Mlimani City, vinginevyo varangati,
Kabidi nijikung’ute, ‘sije kukuudhi switi,
Nami pesa nikakopa, nguo uweze nunua.
Ukataka simu kali, bei yake milioni,
Tena ukataka mbili, zote ziwe iPhone,
Waijua yangu hali, lakini hatwelewani,
Simu hizo nimekupa, bado wataka vingine.
Ukataka iPad, laptop huitaki,
Nami nikajitahidi, nikakopa pesa benki,
Nikuridhishe waridi, moyoni ‘lotamalaki,
Wasema huna furaha, bado sana kuridhika.
Ndege ukataka panda, tena ya Lufthansa,
Eti unachokipenda, kutalii Ufaransa,
Moyo sasa wanidunda, utadhani nina kansa,
Sikai nikatulia, mahabuba huridhiki.
Nimefanya kila jambo, nadhani nakuridhisha,
Kumbe wafata mkumbo, wapo wanokufundisha,
Nateseka joto tumbo, mwenzangu unajirusha,
Nini zaidi nifanye, nawe uache nitesa?
Kingine nikufanyie, ambacho utaridhika,
Niambie nitulie, nimechoka kuteseka,
Nifanyeje uridhike, nambie basi nijue.
Ulitaka yako nyumba, nyumba nayo nikajenga,
Mkopo nikaubamba, wewe uache kupanga,
Ukakataa Kibamba, hutaki wala Ukonga,
Ukataka Mikocheni, nikakopa uridhike.
Nikasema njoo Mbeya, haraka ukakataa,
Ukadai ni kubaya, wataka kuishi Dar,
Nami nikasema haya, nikuridhishe haswaa,
Bado wataka Ulaya, Dar hapajakufaa.
Mara ukataka gari, huzitaki daladala,
Tena gari la fahari, hutaki hizo Corolla,
Nikuridhishe vizuri, nikaenda kopa hela,
Gari umeshalipata, wasema hujaridhika.
Nguo nzuri uzipate, likawa lako sharti,
Tena Mlimani City, vinginevyo varangati,
Kabidi nijikung’ute, ‘sije kukuudhi switi,
Nami pesa nikakopa, nguo uweze nunua.
Ukataka simu kali, bei yake milioni,
Tena ukataka mbili, zote ziwe iPhone,
Waijua yangu hali, lakini hatwelewani,
Simu hizo nimekupa, bado wataka vingine.
Ukataka iPad, laptop huitaki,
Nami nikajitahidi, nikakopa pesa benki,
Nikuridhishe waridi, moyoni ‘lotamalaki,
Wasema huna furaha, bado sana kuridhika.
Ndege ukataka panda, tena ya Lufthansa,
Eti unachokipenda, kutalii Ufaransa,
Moyo sasa wanidunda, utadhani nina kansa,
Sikai nikatulia, mahabuba huridhiki.
Nimefanya kila jambo, nadhani nakuridhisha,
Kumbe wafata mkumbo, wapo wanokufundisha,
Nateseka joto tumbo, mwenzangu unajirusha,
Nini zaidi nifanye, nawe uache nitesa?
Tuesday, October 25, 2011
Pole sana Shaaban
Salamu zangu natuma, kwako kipenzi rafiki,
Hali yangu mimi njema, nipo katika mikiki,
Ninamwomba Mungu mwema, akutoe kwenye dhiki,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Hakika nimeshituka, habari kuisikia,
Jasho tele kunitoka, nikatamani kulia,
Kweli nimesikitika, hilo lililotukia,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Rafiki nimeumia, siwezi kuelezea,
Pindi niliposikia, haya yaliyotokea,
Mola ‘takusaidia, twazidi kukuombea,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Twashukuru umepona, ingawa umeumia,
Twafurahi kukuona, hasa yako familia,
Tunamwomba Maulana, afya akakujalia,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Uzima ndiyo muhimu, ndani ya hii dunia,
Daima yatulazimu, huo kuupigania,
Tutimize majukumu, yanayotuangalia,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Mola atakujalia, uweze pona haraka,
Maisha kupigania, kwa kuzidi chakarika,
Mola twa’tumainia, akupe zake baraka,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Shairi hili ni maalumu kwa rafiki yangu na mwanablog mwenzangu Shaban Kaluse aliyepata ajali ya kugongwa na gari leo asubuhi wakati akielekea kazini. Ninamwombe kupona haraka kwa mkono aliovunjika na maumivu mengine aliyoyapata.
Hali yangu mimi njema, nipo katika mikiki,
Ninamwomba Mungu mwema, akutoe kwenye dhiki,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Hakika nimeshituka, habari kuisikia,
Jasho tele kunitoka, nikatamani kulia,
Kweli nimesikitika, hilo lililotukia,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Rafiki nimeumia, siwezi kuelezea,
Pindi niliposikia, haya yaliyotokea,
Mola ‘takusaidia, twazidi kukuombea,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Twashukuru umepona, ingawa umeumia,
Twafurahi kukuona, hasa yako familia,
Tunamwomba Maulana, afya akakujalia,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Uzima ndiyo muhimu, ndani ya hii dunia,
Daima yatulazimu, huo kuupigania,
Tutimize majukumu, yanayotuangalia,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Mola atakujalia, uweze pona haraka,
Maisha kupigania, kwa kuzidi chakarika,
Mola twa’tumainia, akupe zake baraka,
Pole sana Shaaban, ajali ilokufika.
Shairi hili ni maalumu kwa rafiki yangu na mwanablog mwenzangu Shaban Kaluse aliyepata ajali ya kugongwa na gari leo asubuhi wakati akielekea kazini. Ninamwombe kupona haraka kwa mkono aliovunjika na maumivu mengine aliyoyapata.
Thursday, October 20, 2011
Mpenzi karibu Mbeya
Fanya hima fanya mwaya, uje kunitembelea,
Mie nakusubiriya, moyo wenda peapea,
Mpenzi ufike Mbeya, hamu nawe yazidia,
Mpenzi karibu Mbeya.
Ni kuzuri sana Mbeya, mwenyewe tafurahia,
Wacha maneno mabaya, eti hakujatulia,
Maneno yanowapwaya, mji wautamania,
Mpenzi karibu Mbeya.
Mbeya ni neema tupu, ukija utachanua,
Vyakula wajaza kapu, maradhi hutougua,
Hata ukipenda supu, kuipika ninajua,
Mpenzi karibu Mbeya.
Ardhi ina rutuba, mazao yajiotea,
Utavijaza vibaba, neema waogelea,
Kwetu wala na kushiba, mwenyewe kuchekelea,
Mpenzi karibu Mbeya.
Mbeya utakula ndizi, na makatapera pia,
Mihogo navyo viazi, matembele na bamia,
Wali usotaka nazi, wanoga ninakwambia,
Mpenzi karibu Mbeya.
Mbeya kila kitu kipo, hakika tafurahia,
Maembe hadi maepo, hata na kakao pia,
Na magimbi nayo yapo, wewe yakusubiria,
Mpenzi karibu Mbeya.
Miwa yake ni mitamu, na utaing'ang'ania,
Kwani haiishi hamu, hakika ninakwambia,
Kwakufaa sana humu, hima usijekawia,
Mpenzi karibu Mbeya.
Hali yake burudani, hewa iliyotulia,
Kijibaridi fulani, mwili kichosisimua,
Wala huhitaji feni, kifua kuharibia,
Mpenzi karibu Mbeya.
Mpenzi nakusubiri, Mbeya ndo panakufaa,
Njoo mji ni mzuri, na ukija utang'aa,
Hakika utanawiri, upendeze kila saa,
Mpenzi karibu Mbeya.
Mie nakusubiriya, moyo wenda peapea,
Mpenzi ufike Mbeya, hamu nawe yazidia,
Mpenzi karibu Mbeya.
Ni kuzuri sana Mbeya, mwenyewe tafurahia,
Wacha maneno mabaya, eti hakujatulia,
Maneno yanowapwaya, mji wautamania,
Mpenzi karibu Mbeya.
Mbeya ni neema tupu, ukija utachanua,
Vyakula wajaza kapu, maradhi hutougua,
Hata ukipenda supu, kuipika ninajua,
Mpenzi karibu Mbeya.
Ardhi ina rutuba, mazao yajiotea,
Utavijaza vibaba, neema waogelea,
Kwetu wala na kushiba, mwenyewe kuchekelea,
Mpenzi karibu Mbeya.
Mbeya utakula ndizi, na makatapera pia,
Mihogo navyo viazi, matembele na bamia,
Wali usotaka nazi, wanoga ninakwambia,
Mpenzi karibu Mbeya.
Mbeya kila kitu kipo, hakika tafurahia,
Maembe hadi maepo, hata na kakao pia,
Na magimbi nayo yapo, wewe yakusubiria,
Mpenzi karibu Mbeya.
Miwa yake ni mitamu, na utaing'ang'ania,
Kwani haiishi hamu, hakika ninakwambia,
Kwakufaa sana humu, hima usijekawia,
Mpenzi karibu Mbeya.
Hali yake burudani, hewa iliyotulia,
Kijibaridi fulani, mwili kichosisimua,
Wala huhitaji feni, kifua kuharibia,
Mpenzi karibu Mbeya.
Mpenzi nakusubiri, Mbeya ndo panakufaa,
Njoo mji ni mzuri, na ukija utang'aa,
Hakika utanawiri, upendeze kila saa,
Mpenzi karibu Mbeya.
Tuesday, October 18, 2011
Mwenziyo sinayo khali
Muhashamu muhashamu, ujumbe nakutumia,
Pokea zangu salamu, za mashamshamu pia,
Nimepatwa na wazimu, siachi kukuwazia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Kama mapenzi ni sumu, basi imeniingia,
Nakesha mang’amung’amu, wewe kukufikiria,
Yanienda kasi damu, moyo h’utaki tulia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Moyo ‘ngekuwa na zamu, nawe ningekupatia,
Uzionje zilo humu, zilivyojaa hisia,
Halisi zilizo tamu, wewe nizo kupatia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Naganda kama sanamu, wewe ninakungojea,
Zingali siku zatimu, moyo khali wasemea,
Kwa pendo hili adhimu, wewe tuu kukupea,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Wao wanonituhumu, hawawezi nisumbua,
Kukupenda ‘melazimu, vinginevyo naugua,
Ungali yangu naumu, hapa chini yake jua,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Penzi lisilo awamu, kusema litapungua,
Penzi daima dawamu, moyo wangu we chukua,
Kukupenda ni swaumu, pendo nal’ombea dua,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Sihesabu tarakimu, penzi linavyozidia,
Bali ni mastakimu, hakuna ‘nokufikia,
Hakuna wa kukaimu, nafasi ‘nokupatia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Uzuri wako adimu, wengi wanaulilia,
Wazikoleza fahamu, daima nakuwazia,
Kukupenda ni jukumu, mwingine sitomwachia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Kwako siishiwi hamu, kila siku wazidia,
Mapishi yako matamu, mtu sito’bakishia,
Hakika wewe mwalimu, cheti nakutunukia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Beti kumi zimetimu, wewe nimekwandikia,
Nitapiga hata simu, maneno nikakwambia,
Daima nitajihimu, wimbo nikakuimbia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Pokea zangu salamu, za mashamshamu pia,
Nimepatwa na wazimu, siachi kukuwazia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Kama mapenzi ni sumu, basi imeniingia,
Nakesha mang’amung’amu, wewe kukufikiria,
Yanienda kasi damu, moyo h’utaki tulia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Moyo ‘ngekuwa na zamu, nawe ningekupatia,
Uzionje zilo humu, zilivyojaa hisia,
Halisi zilizo tamu, wewe nizo kupatia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Naganda kama sanamu, wewe ninakungojea,
Zingali siku zatimu, moyo khali wasemea,
Kwa pendo hili adhimu, wewe tuu kukupea,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Wao wanonituhumu, hawawezi nisumbua,
Kukupenda ‘melazimu, vinginevyo naugua,
Ungali yangu naumu, hapa chini yake jua,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Penzi lisilo awamu, kusema litapungua,
Penzi daima dawamu, moyo wangu we chukua,
Kukupenda ni swaumu, pendo nal’ombea dua,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Sihesabu tarakimu, penzi linavyozidia,
Bali ni mastakimu, hakuna ‘nokufikia,
Hakuna wa kukaimu, nafasi ‘nokupatia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Uzuri wako adimu, wengi wanaulilia,
Wazikoleza fahamu, daima nakuwazia,
Kukupenda ni jukumu, mwingine sitomwachia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Kwako siishiwi hamu, kila siku wazidia,
Mapishi yako matamu, mtu sito’bakishia,
Hakika wewe mwalimu, cheti nakutunukia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
Beti kumi zimetimu, wewe nimekwandikia,
Nitapiga hata simu, maneno nikakwambia,
Daima nitajihimu, wimbo nikakuimbia,
Mwenziyo sinayo khali, sijiwezi juu yako.
maudhui
mapenzi
Tuesday, October 11, 2011
Ningoje hadi lini?
Mwenzio bado nangoja, ahadi uliyonipa,
Hali yangu reja reja, wala si ya kuchumpa,
Nilishazitowa hoja, basi sinitowe kapa,
Ningoje hadi lini?
Nambie lini wakati, utaponipa majibu,
Moyo kizungumkuti, kwani waupa adhabu,
Hauna tena ukuti, wakusubiri tabibu,
Ningoje hadi lini?
Kwamba nivute subira, nishasubiria sana,
Hadi hali yadorora, usiku nao mchana,
Nitoe kwenye madhara, nishazama kwacho kina,
Ningoje hadi lini?
Jibulo lanipa hamu, hamu ya kulisikia,
Ila sinipe wazimu, chonde sinipe umia,
Likoleze uhashamu, nifurahie dunia,
Ningoje hadi lini?
Usiku wote silali, wewe nakufikiria,
Mwenzio sinayo hali, jibu ninaliwazia,
Chonde mara mbili mbili, niepushie kulia,
Ningoje hadi lini?
Ninakonda ninakonda, nipo hoi taabani,
Chakula kinanishinda, hakinipiti kooni,
Fanya hima kunikanda, unondowe taabuni,
Ningoje hadi lini?
Nieleze yako nia, unondoe wasiwasi,
Nini unadhamiria, mana moyo wenda kasi,
Mwenzio nasubiria, chonde nijibu upesi,
Nimeshangoja sana.
Hali yangu reja reja, wala si ya kuchumpa,
Nilishazitowa hoja, basi sinitowe kapa,
Ningoje hadi lini?
Nambie lini wakati, utaponipa majibu,
Moyo kizungumkuti, kwani waupa adhabu,
Hauna tena ukuti, wakusubiri tabibu,
Ningoje hadi lini?
Kwamba nivute subira, nishasubiria sana,
Hadi hali yadorora, usiku nao mchana,
Nitoe kwenye madhara, nishazama kwacho kina,
Ningoje hadi lini?
Jibulo lanipa hamu, hamu ya kulisikia,
Ila sinipe wazimu, chonde sinipe umia,
Likoleze uhashamu, nifurahie dunia,
Ningoje hadi lini?
Usiku wote silali, wewe nakufikiria,
Mwenzio sinayo hali, jibu ninaliwazia,
Chonde mara mbili mbili, niepushie kulia,
Ningoje hadi lini?
Ninakonda ninakonda, nipo hoi taabani,
Chakula kinanishinda, hakinipiti kooni,
Fanya hima kunikanda, unondowe taabuni,
Ningoje hadi lini?
Nieleze yako nia, unondoe wasiwasi,
Nini unadhamiria, mana moyo wenda kasi,
Mwenzio nasubiria, chonde nijibu upesi,
Nimeshangoja sana.
Wednesday, September 28, 2011
Siku nyingi sana
Hakika sijaandika, nanyi hamjanisikia,
Ghafula nikakatika, bila hata kuwambia,
Wengi mkahamanika, nini kimenitukia,
Maswali yakawashika, vipi nimewakimbia,
Siku nyingi sana!
Wapi nilikofichika, hakuna wa kuwa'ambia,
Wapo walokasirika, bakora kunishikia,
Shimoni leo natoka, sitaki kosa rudia,
Mpate kuburudika, yote lowakusanyia,
Siku nyingi sana!
Nyote hapa kusanyika, nianze wahadithia,
Kunako zangu pilika, yote nilojionea,
Hakika tafurahika, khasira kuwaishia,
Hatungoji pambazuka, hivi ndo twajianzia,
Paukwa......!!!
Ghafula nikakatika, bila hata kuwambia,
Wengi mkahamanika, nini kimenitukia,
Maswali yakawashika, vipi nimewakimbia,
Siku nyingi sana!
Wapi nilikofichika, hakuna wa kuwa'ambia,
Wapo walokasirika, bakora kunishikia,
Shimoni leo natoka, sitaki kosa rudia,
Mpate kuburudika, yote lowakusanyia,
Siku nyingi sana!
Nyote hapa kusanyika, nianze wahadithia,
Kunako zangu pilika, yote nilojionea,
Hakika tafurahika, khasira kuwaishia,
Hatungoji pambazuka, hivi ndo twajianzia,
Paukwa......!!!
Thursday, September 1, 2011
Moyo wangu
Usiuache mpweke, maumivu kuufika,
Siufanye uteseke, machozi yakanitoka,
Ufanye ufarijike, upe moyo uhakika,
Moyo wangu.
Upatie unafuu, upunguzie mawazo,
Uweke daima juu, sikalie matatizo,
Siupige kwa miguu, na kuupa mizevezo,
Moyo wangu.
Uondolee karaha, siuweke taabuni,
Ufanye kuwa na raha, sizamishe majonzini,
Utawalwe na furaha, cheko tupu maishani,
Moyo wangu.
Usiutendee hivyo, moyo wangu taumia,
Ukitenda ndivyo sivyo, kitanzi utautia,
Vyovyote vile iwavyo, elewa wakuzimia,
Moyo wangu.
Siufanye uteseke, machozi yakanitoka,
Ufanye ufarijike, upe moyo uhakika,
Moyo wangu.
Upatie unafuu, upunguzie mawazo,
Uweke daima juu, sikalie matatizo,
Siupige kwa miguu, na kuupa mizevezo,
Moyo wangu.
Uondolee karaha, siuweke taabuni,
Ufanye kuwa na raha, sizamishe majonzini,
Utawalwe na furaha, cheko tupu maishani,
Moyo wangu.
Usiutendee hivyo, moyo wangu taumia,
Ukitenda ndivyo sivyo, kitanzi utautia,
Vyovyote vile iwavyo, elewa wakuzimia,
Moyo wangu.
maudhui
mapenzi
Friday, August 26, 2011
Moyoni unatawala
Nasema kila wasaa, maneno nitarudia,
Kamwe sitoyakataa, haya nayosimulia,
Moyoni ushanijaa, moyoni ushaingia,
Moyoni unatawala.
Moyoni mwangu wang'aa, tuli tuli watulia,
Nakupenda wewe maa, hakuna 'nokufikia,
Neno langu si hadaa, leo kweli nakwambia,
Moyoni unatawala.
Silali wala kukaa, pasina kufikiria,
Wewe ndo wewe haswaa, ndotoni naenijia,
Moyo tanienda paa, siku ukinikimbia,
Moyoni unatawala.
Wengine wote kataa, wache kukufatilia,
Mwambie wazi hataa, moyoni 'jakuingia,
Wabaki wakishangaa, sisi tukifurahia,
Moyoni unatawala.
Unatawala kiwaa, dobo na numbula pia,
Bora nikae na njaa, ila kwako kutulia,
Wewe hunayo mawaa, kwa raha nonipatia,
Moyoni unatawala.
Kamwe sitoyakataa, haya nayosimulia,
Moyoni ushanijaa, moyoni ushaingia,
Moyoni unatawala.
Moyoni mwangu wang'aa, tuli tuli watulia,
Nakupenda wewe maa, hakuna 'nokufikia,
Neno langu si hadaa, leo kweli nakwambia,
Moyoni unatawala.
Silali wala kukaa, pasina kufikiria,
Wewe ndo wewe haswaa, ndotoni naenijia,
Moyo tanienda paa, siku ukinikimbia,
Moyoni unatawala.
Wengine wote kataa, wache kukufatilia,
Mwambie wazi hataa, moyoni 'jakuingia,
Wabaki wakishangaa, sisi tukifurahia,
Moyoni unatawala.
Unatawala kiwaa, dobo na numbula pia,
Bora nikae na njaa, ila kwako kutulia,
Wewe hunayo mawaa, kwa raha nonipatia,
Moyoni unatawala.
maudhui
mapenzi
Thursday, August 25, 2011
Sauti yangu
Ninataka kuipaza, ilokaza,
Kotekote kueneza, nacho waza,
Wote muje kusikiza, mkiweza,
Nayoeleza!
Kuna mambo yanikwaza, yanumiza,
Kukimya sitokuweza, tonyamaza,
Silali kucha nawaza, nahasiza,
Wanichagiza!
Niaje yazidi oza, yachakaza,
Vyote vyema wamaliza, wakombeza,
Ni lini watabakiza, wandekeza,
Mauzauza!
Sauti yangu napaza, nakataza,
Mola fimbo wacharaza, tena kaza,
Wajutie wao kwanza, wamaliza,
Wavokombeza!
Kotekote kueneza, nacho waza,
Wote muje kusikiza, mkiweza,
Nayoeleza!
Kuna mambo yanikwaza, yanumiza,
Kukimya sitokuweza, tonyamaza,
Silali kucha nawaza, nahasiza,
Wanichagiza!
Niaje yazidi oza, yachakaza,
Vyote vyema wamaliza, wakombeza,
Ni lini watabakiza, wandekeza,
Mauzauza!
Sauti yangu napaza, nakataza,
Mola fimbo wacharaza, tena kaza,
Wajutie wao kwanza, wamaliza,
Wavokombeza!
maudhui
siasa
Wednesday, August 3, 2011
Waambie
Ukiwa nao waambie, maneno yawafikie,
Jitahidi wasikie, ujumbe uwafikie,
Ili wasiulizie, bure wasijisumbue,
Waambie hao wote, umenichagua mie.
Wakate vyao vilimi, ikibidi waumie,
Sema wanipenda mimi, waambie wasikie,
Sema mara kumi kumi, sauti iwafikie,
Waambie hao wote, kuwa wanipenda mie.
Hawapendi ninajua, we’ waache waumie,
Wivu unawasumbua, watamani watibue,
Sie tunaomba dua, Muumba atujalie,
Waambie hao wote, umenichagua mi.
Waambie wafitini, na chuki zao walie,
Na wala wasijihini, hawatotuweza sie,
Tumeshazama dimbwini, tumeshanogewa sie,
Waambie hao wote, kuwa wanipenda mie.
We’ waambie mpenzi, yawachome waumie,
Na zidisha kunienzi, ili nifaidi mie,
Niyafaidi mapenzi, pendolo nijivunie,
Waambie hao wote, umenichagua mie.
Mpenzi we’ u mzuri, yeyote asikwambie,
Unanipa ufahari, na raha usisikie,
Nasi twombeane kheri, mapenzi yetu yakue,
Waambie hao wote, kuwa wanipenda mie.
Waseme hata wachoke, wacha tupendane sie,
Kote kote wazunguke, watashindwa wajijue,
Na watake wasitake, siye tuyafurahie,
Waambie hao wote, umenichagua mie.
Hata washikwe na wivu, wenyewe nd’o waumie,
Sie twala zetu mbivu, watwache tufurahie,
Wayapate maumivu, mioyoni waumie,
Waambie hao wote, kuwa wanipenda mie.
Watayasema mchana, ngoja giza liingie,
Watalala tena sana, na ndoto ziwasumbue,
Tutazidi kupendana, watakoma wakomae,
Waambie hao wote, umenichagua mie.
Hujachagua mwingine, isipokuwa ni mie,
Hivyo nasi tupendane, raha na tujipatie,
Wao wahangaishane, sie wasitufikie,
Waambie hao wote, kuwa wanipenda mie.
Waambie wasikie, nenolo liwainngie,
Tena wasijisumbue, mapenzi ni yetu sie,
Waumie siumie, tunajivinjari sie,
Waambie hao wote, umenichagua mie.
Waambie wasikie!
Jitahidi wasikie, ujumbe uwafikie,
Ili wasiulizie, bure wasijisumbue,
Waambie hao wote, umenichagua mie.
Wakate vyao vilimi, ikibidi waumie,
Sema wanipenda mimi, waambie wasikie,
Sema mara kumi kumi, sauti iwafikie,
Waambie hao wote, kuwa wanipenda mie.
Hawapendi ninajua, we’ waache waumie,
Wivu unawasumbua, watamani watibue,
Sie tunaomba dua, Muumba atujalie,
Waambie hao wote, umenichagua mi.
Waambie wafitini, na chuki zao walie,
Na wala wasijihini, hawatotuweza sie,
Tumeshazama dimbwini, tumeshanogewa sie,
Waambie hao wote, kuwa wanipenda mie.
We’ waambie mpenzi, yawachome waumie,
Na zidisha kunienzi, ili nifaidi mie,
Niyafaidi mapenzi, pendolo nijivunie,
Waambie hao wote, umenichagua mie.
Mpenzi we’ u mzuri, yeyote asikwambie,
Unanipa ufahari, na raha usisikie,
Nasi twombeane kheri, mapenzi yetu yakue,
Waambie hao wote, kuwa wanipenda mie.
Waseme hata wachoke, wacha tupendane sie,
Kote kote wazunguke, watashindwa wajijue,
Na watake wasitake, siye tuyafurahie,
Waambie hao wote, umenichagua mie.
Hata washikwe na wivu, wenyewe nd’o waumie,
Sie twala zetu mbivu, watwache tufurahie,
Wayapate maumivu, mioyoni waumie,
Waambie hao wote, kuwa wanipenda mie.
Watayasema mchana, ngoja giza liingie,
Watalala tena sana, na ndoto ziwasumbue,
Tutazidi kupendana, watakoma wakomae,
Waambie hao wote, umenichagua mie.
Hujachagua mwingine, isipokuwa ni mie,
Hivyo nasi tupendane, raha na tujipatie,
Wao wahangaishane, sie wasitufikie,
Waambie hao wote, kuwa wanipenda mie.
Waambie wasikie, nenolo liwainngie,
Tena wasijisumbue, mapenzi ni yetu sie,
Waumie siumie, tunajivinjari sie,
Waambie hao wote, umenichagua mie.
Waambie wasikie!
maudhui
mapenzi
Saturday, July 30, 2011
Muwe kwangu marafiki
Nahitaji marafiki,
Ambao watanijali, bila unafiki,
Si kwa ajili ya mali, nami nina dhiki,
Bali kwa pendo la kweli, lisilo na taki,
Muwe kwangu marafiki.
Nahitaji marafiki,
Mie ninatawasali, wawe hata laki,
Sitofanya tasihili, kutaka lahiki,
Niombe ardhilhali, kukosa sitaki,
Muwe kwangu marafiki.
Nahitaji marafiki,
Ninamuomba Jalali, nipate lukuki,
Watoke kote mahali, iwe halaiki,
Nitawafanya halili, watatamalaki,
Muwe kwangu marafiki.
Nahitaji marafiki,
Ninawahitaji kweli, muwe marafiki,
Najua mtajamali, ‘sininyweshe hiyo siki,
Siyo maneno makali, nikiishindwa mikiki,
Muwe kwangu marafiki.
Nahitaji marafiki,
Tupendane kila hali, wenye tamaa sitaki,
Naahidi kuwajali, kwazo raha nazo dhiki,
Pamoja tustahimili, yayo maisha mikiki,
Muwe kwangu marafiki.
Nahitaji marafiki,
Nitawafanya aghali, fakhari kuwamiliki,
Duwa zangu mbili mbili, mpate kile na hiki,
Mola wangu tafadhali, wawe wengi halaiki,
Muwe kwangu marafiki.
Ambao watanijali, bila unafiki,
Si kwa ajili ya mali, nami nina dhiki,
Bali kwa pendo la kweli, lisilo na taki,
Muwe kwangu marafiki.
Nahitaji marafiki,
Mie ninatawasali, wawe hata laki,
Sitofanya tasihili, kutaka lahiki,
Niombe ardhilhali, kukosa sitaki,
Muwe kwangu marafiki.
Nahitaji marafiki,
Ninamuomba Jalali, nipate lukuki,
Watoke kote mahali, iwe halaiki,
Nitawafanya halili, watatamalaki,
Muwe kwangu marafiki.
Nahitaji marafiki,
Ninawahitaji kweli, muwe marafiki,
Najua mtajamali, ‘sininyweshe hiyo siki,
Siyo maneno makali, nikiishindwa mikiki,
Muwe kwangu marafiki.
Nahitaji marafiki,
Tupendane kila hali, wenye tamaa sitaki,
Naahidi kuwajali, kwazo raha nazo dhiki,
Pamoja tustahimili, yayo maisha mikiki,
Muwe kwangu marafiki.
Nahitaji marafiki,
Nitawafanya aghali, fakhari kuwamiliki,
Duwa zangu mbili mbili, mpate kile na hiki,
Mola wangu tafadhali, wawe wengi halaiki,
Muwe kwangu marafiki.
Thursday, July 28, 2011
Mimi kwako nimetuwa
Ndege daima hutua, kwenye mti apendao,
Ndege hatojisumbua, mti auchukiao,
Ndege yeye huchagua, mmea autakao,
Mimi kwako nimetuwa.
Nimeruka miti yote, nimetuwa kwako wewe,
Nipe moyo wako wote, ili kwangu uchanuwe,
Raha kamili nipate, nisiende kwinginewe,
Mimi kwako nimetuwa.
Kwako wewe nimetuwa, mi’ sijamwona mwingine,
Wewe nimekuchaguwa, nahitaji tupendane,
Moyo wangu nautowa, siupeleki kwingine,
Mimi kwako nimetuwa.
Kutuwa nimeridhika, nimeamua mwenyewe,
Ninasema kwa hakika, napenda unielewe,
Mimi kwako nimefika, sifikiri kwinginewe,
Mimi kwako nimetuwa.
Kwako wewe sina shaka, moyo umenituwama,
Namwomba wetu Rabuka, atujalie salama,
Tufurahi na kucheka, pote panapo uzima,
Mimi kwako nimetuwa.
Nawe pia usihofu, kwani u chaguo langu,
Nikupende maradufu, wewe u sehemu yangu,
Naahidi hutokifu, kwenye huu ulimwengu,
Mimi kwako nimetuwa.
Wazia kuhusu mimi, ukihitaji furaha,
Lilo langu sikunyimi, nitakupa lilo weha,
Makumi kwayo makumi, daima uwe na raha,
Mimi kwako nimetuwa.
Mimi nd’o unieleze, yale yanaokusibu,
Kwa upendo nisikize, nitowe yalo majibu,
Njia nikuelekeze, we’ ulo wangu muhibu,
Mimi kwako nimetuwa.
Mimi ndiye ndege wako, kwako nimekwisha tuwa,
Kokote kule twendako, tupendane tavyokuwa,
Tuzishinde chokochoko, zao wanojisumbuwa,
Mimi kwako nimetuwa.
Ndege hatojisumbua, mti auchukiao,
Ndege yeye huchagua, mmea autakao,
Mimi kwako nimetuwa.
Nimeruka miti yote, nimetuwa kwako wewe,
Nipe moyo wako wote, ili kwangu uchanuwe,
Raha kamili nipate, nisiende kwinginewe,
Mimi kwako nimetuwa.
Kwako wewe nimetuwa, mi’ sijamwona mwingine,
Wewe nimekuchaguwa, nahitaji tupendane,
Moyo wangu nautowa, siupeleki kwingine,
Mimi kwako nimetuwa.
Kutuwa nimeridhika, nimeamua mwenyewe,
Ninasema kwa hakika, napenda unielewe,
Mimi kwako nimefika, sifikiri kwinginewe,
Mimi kwako nimetuwa.
Kwako wewe sina shaka, moyo umenituwama,
Namwomba wetu Rabuka, atujalie salama,
Tufurahi na kucheka, pote panapo uzima,
Mimi kwako nimetuwa.
Nawe pia usihofu, kwani u chaguo langu,
Nikupende maradufu, wewe u sehemu yangu,
Naahidi hutokifu, kwenye huu ulimwengu,
Mimi kwako nimetuwa.
Wazia kuhusu mimi, ukihitaji furaha,
Lilo langu sikunyimi, nitakupa lilo weha,
Makumi kwayo makumi, daima uwe na raha,
Mimi kwako nimetuwa.
Mimi nd’o unieleze, yale yanaokusibu,
Kwa upendo nisikize, nitowe yalo majibu,
Njia nikuelekeze, we’ ulo wangu muhibu,
Mimi kwako nimetuwa.
Mimi ndiye ndege wako, kwako nimekwisha tuwa,
Kokote kule twendako, tupendane tavyokuwa,
Tuzishinde chokochoko, zao wanojisumbuwa,
Mimi kwako nimetuwa.
maudhui
mapenzi
Tuesday, July 26, 2011
Hadi lini?
Ahadi mtazitowa, msizo zitekeleza?
Mambo mtayazodowa, na kisha kuyachagiza?
Tazidi pata madowa, kisha kujibaraguza?
Hadi lini, mtwambie!
Takumbata mafisadi, maovu mkayakuza?
Mtafanya makusudi, wananchi kuwapuza?
Mtaacha ukaidi, ukweli kutueleza?
Hadi lini, mtwambie!
Taleta maendeleo, siyo kujilimbikiza?
Takemea nyendo zao, wale wanotuumiza?
Taviondoa vilio, wagonjwa wan'oj'uguza?
Hadi lini, mtwambie!
Tuwangoje hadi lini, maana mwatuchokeza,
Semeni haya semeni, twataka wasikiliza,
Mwatutesa mioyoni, vidonda vazidi oza,
Hadi lini, mtwambie!
Hadi lini mtwambie, sana 'metunyong'onyeza,
Msitwache tuumie, siku tawatokomeza,
Yafaa mtusikie, nasi mkaja tuguza,
Hadi lini, mtwambie!
Mbona hamna huruma, tamaa tawamaliza,
Mwachota bila kupima, hamjui kubakiza,
Lini mtakuwa wema, taifa kutongamiza,
Hadi lini, mtwambie!
Hatukufundishwa hivyo, Mwalimu 'livyo'lekeza,
Hivyo sasa mfanyavyo, somo mshalipuuza,
Hivi ndivyo mpendavyo, maadili yalooza,
Hadi lini, mtwambie!
Kila siku twawambia, mngali mwajendekeza,
Mmeharibu tabia, watot'wenu mwawafunza,
Nao weharibikia, kila kitu wakombeza,
Hadi lini, mtwambie!
Nani huyo kawaroga, tuje tukamcheteza,
Maana mwamwaga mboga, ugali mwahanikiza,
Mtamaliza maboga, mkabaki mwamwagaza,
Hadi lini, mtwambie!
Hadi lini mtwambie, tumechoka kungojeza,
Hadi lini twandikie, msopenda kusikiza,
Aibu iwaingie, ili muje kutweleza,
Hadi lini, twambieni!
Mambo mtayazodowa, na kisha kuyachagiza?
Tazidi pata madowa, kisha kujibaraguza?
Hadi lini, mtwambie!
Takumbata mafisadi, maovu mkayakuza?
Mtafanya makusudi, wananchi kuwapuza?
Mtaacha ukaidi, ukweli kutueleza?
Hadi lini, mtwambie!
Taleta maendeleo, siyo kujilimbikiza?
Takemea nyendo zao, wale wanotuumiza?
Taviondoa vilio, wagonjwa wan'oj'uguza?
Hadi lini, mtwambie!
Tuwangoje hadi lini, maana mwatuchokeza,
Semeni haya semeni, twataka wasikiliza,
Mwatutesa mioyoni, vidonda vazidi oza,
Hadi lini, mtwambie!
Hadi lini mtwambie, sana 'metunyong'onyeza,
Msitwache tuumie, siku tawatokomeza,
Yafaa mtusikie, nasi mkaja tuguza,
Hadi lini, mtwambie!
Mbona hamna huruma, tamaa tawamaliza,
Mwachota bila kupima, hamjui kubakiza,
Lini mtakuwa wema, taifa kutongamiza,
Hadi lini, mtwambie!
Hatukufundishwa hivyo, Mwalimu 'livyo'lekeza,
Hivyo sasa mfanyavyo, somo mshalipuuza,
Hivi ndivyo mpendavyo, maadili yalooza,
Hadi lini, mtwambie!
Kila siku twawambia, mngali mwajendekeza,
Mmeharibu tabia, watot'wenu mwawafunza,
Nao weharibikia, kila kitu wakombeza,
Hadi lini, mtwambie!
Nani huyo kawaroga, tuje tukamcheteza,
Maana mwamwaga mboga, ugali mwahanikiza,
Mtamaliza maboga, mkabaki mwamwagaza,
Hadi lini, mtwambie!
Hadi lini mtwambie, tumechoka kungojeza,
Hadi lini twandikie, msopenda kusikiza,
Aibu iwaingie, ili muje kutweleza,
Hadi lini, twambieni!
maudhui
siasa
Subscribe to:
Posts (Atom)
